Methali 31:4-7
Methali 31:4-7 Biblia Habari Njema (BHN)
Haifai ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai, wala wakuu kutamani vileo. Wakinywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu. Mpe kileo mtu anayekufa, wape divai wale wenye huzuni tele; wanywe na kusahau umaskini wao, wasikumbuke tena taabu yao.
Methali 31:4-7 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Ee Lemueli, kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme; Wala haifai wakuu waseme, Kiko wapi kileo? Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni. Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini. Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake.
Methali 31:4-7 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Ee Lemueli, kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme; Wala haifai wakuu waseme, Ki wapi kileo? Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni. Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini. Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake.
Methali 31:4-7 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
“Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo, wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa. Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu, Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.