Yobu 36:27-33
Yobu 36:27-33 Biblia Habari Njema (BHN)
Yeye huyavuta kwake maji ya bahari, na kutoka ukungu hufanya matone ya mvua. Huyafanya mawingu yanyeshe mvua, na kuwatiririshia binadamu kwa wingi. Nani ajuaye jinsi mawingu yatandavyo, au jinsi radi ingurumavyo angani kwake? Yeye huutandaza umeme wake kumzunguka, na kuvifunika vilindi vya bahari. Kwa mvua huwalisha watu na kuwapatia chakula kwa wingi. Huukamata umeme kwa mikono yake, kisha hulenga nao shabaha, Radi hutangaza ujio wake Mungu, hata wanyama hujua kwamba anakuja.
Yobu 36:27-33 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Maana yeye huvuta juu matone ya maji, Yamwagikayo katika mvua kutoka ukungu wake; Ambayo mawingu yainyesha Na kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi. Naam, mtu aweza kuelewa matandazo ya mawingu, Ngurumo za makao yake? Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke; Naye hufunika vilindi vya bahari. Kwani huwahukumu makabila ya watu kwa njia hizi; Hutoa chakula kwa ukarimu. Yeye huifunika mikono yake kwa umeme; Na kuuagiza shabaha utakayopiga. Mshindo wake hutoa habari zake, Anayewaka hasira juu ya uovu.
Yobu 36:27-33 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Kwani yeye huvuta juu matone ya maji, Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake; Ambayo mawingu yainyesha Na kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi. Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu, Ngurumo za makao yake? Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke; Naye hufunika vilindi vya bahari. Kwani huwahukumu kabila za watu kwa njia hizi; Hutoa chakula kwa ukarimu. Yeye huifunika mikono yake kwa umeme; Na kuuagiza shabaha utakayopiga. Mshindo wake hutoa habari zake, Anayewaka hasira juu ya uovu.
Yobu 36:27-33 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito; mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu. Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake. Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari. Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi. Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake. Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.