Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yobu 37:17-24

Yobu 37:17-24 BHN

Wewe wajiona umevaa nguo za joto sana, wakati upepo wa kusi unaivamia nchi. Je, waweza, kuzitandaza mbingu kama yeye zikawa ngumu kama kioo cha shaba? Tufundishe tutakachomwambia Mungu; maana hoja zetu si wazi, tumo gizani. Je, nani anathubutu kumwambia: Nataka kuongea? Nani aseme apate balaa? “Ghafla mtu hawezi tena kuona waziwazi: Jua limefichika nyuma ya mawingu, na upepo umefagia anga! Mngao mzuri hutokea kaskazini; Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha. Mungu Mwenye Nguvu asiyeweza kufikiwa na mtu, uwezo na uadilifu wake ni mkuu, amejaa wema wala hapotoshi haki kamwe. Kwa hiyo, watu wote humwogopa; yeye hamjali mtu yeyote mwenye kiburi.”

Soma Yobu 37

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Yobu 37:17-24

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha