Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 99

99
Sifa kwa Utukufu wa Mungu
1 # Kut 25:22 BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;
Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.
2BWANA katika Sayuni ni mkuu,
Naye ametukuka juu ya mataifa yote.
3 # Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8 Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa;
Ndiye mtakatifu.
4 # Kum 32:3,4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Mwa 18:25 Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu;
Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili;
Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.
5 # 1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni penye kiti cha miguu yake;
Ndiye mtakatifu.
6Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake,
Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake,
Walipomwita Bwana aliwaitikia;
7 # Kut 19:9; Kut 33:9; Hes 12:5 Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao.
Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.
8 # Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20 Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;
Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe
Ingawa uliwapatiliza matendo yao.
9Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;
Maana BWANA, Mungu wetu, ndiye mtakatifu.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 99: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha