Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 8

8
Utukufu wa Mungu na Hadhi ya Utu
Kwa mwimbishaji: kwa kufuata Gitithi. Zaburi ya Daudi.
1Wewe, MUNGU, Bwana wetu
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
2 # Mt 21:16; 11:25; 1 Kor 1:27 Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao
Umeiweka misingi ya nguvu;
Kwa sababu yao wanaoshindana nawe;
Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.
3 # Zab 44:16; 19:1; Ayu 22:12; Rum 1:20 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako,
Mwezi na nyota ulizoziratibisha;
4 # Ayu 7:17-18; Zab 144:3; Ebr 2:6-8 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,
Na binadamu hata umwangalie?
5Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;
Umemvika taji ya utukufu na heshima;
6 # 1 Kor 15:27; Efe 1:22; Ebr 2:8; Mwa 1:26 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
7Kondoo, na ng’ombe wote pia;
Naam, na wanyama wa kondeni;
8Ndege wa angani, na samaki wa baharini;
Na kila kipitacho njia za baharini.
9 # Ayu 11:7; Zab 35:10 Wewe, MUNGU, Bwana wetu,
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Iliyochaguliwa sasa

Zab 8: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha