Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 6

6
Sala ya Kuponywa Ugonjwa Hatari
Kwa mwimbishaji: kwa ala za muziki zenye nyuzi; kulingana na mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi.
1 # Zab 38:1 BWANA, usinikemee kwa hasira yako,
Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.
2 # Hos 6:1 BWANA, unifadhili, maana ninanyauka;
BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.
3 # Mit 18:14; Mt 26:38 Na nafsi yangu imefadhaika sana;
Na Wewe, BWANA, hata lini?
4BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu,
Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
5 # Zab 30:9 Maana mautini hapana kumbukumbu lako;
Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?
6Nimechoka kwa kuugua kwangu;
Kila usiku nakieleza kitanda changu;
Nalilowesha godoro langu kwa machozi yangu.
7Jicho langu limeharibika kwa masumbufu,
Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.
8 # Mt 7:23; Lk 13:27 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu;
Kwa kuwa BWANA ameisikia sauti ya kilio changu.
9 # Zab 3:4; 31:22; 40:1,2 BWANA ameisikia dua yangu;
BWANA atayatakabali maombi yangu.
10Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,
Watarudi nyuma, kwa ghafula wataaibika.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 6: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha