Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 15

15
Nani Atakaa katika Patakatifu pa Mungu?
Zaburi ya Daudi.
1 # Zab 2:5 BWANA, ni nani atakayekaa
Katika hema yako?
Ni nani atakayefanya maskani yake
Katika kilima chako kitakatifu?
2 # Zab 84:11; Isa 33:15,16 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,
Na kutenda haki.
Asemaye kweli kwa moyo wake,
3Asiyesingizia kwa ulimi wake.
Wala hakumtenda mwenziwe mabaya,
Wala hakumsengenya jirani yake.
4 # Yos 9:18-20 Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa,
Bali huwaheshimu wamchao BWANA
Ingawa ameapa kwa hasara yake,
Hayabadili maneno yake.
5 # Eze 18:8,9 Hakutoa fedha yake apate kula riba,
Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia.
Mtu atendaye mambo hayo
Hataondoshwa milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 15: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha