Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 112

112
Baraka za Mwenye Haki
1Haleluya.
Heri mtu yule amchaye BWANA,
Apendezwaye sana na maagizo yake.
2Wazao wake watakuwa hodari duniani;
Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.
3 # Mit 3:16; 15:6; Isa 33:6; Mt 6:33; 2 Kor 6:10 Nyumbani mwake mna utajiri na mali,
Na haki yake yakaa milele.
4Nuru huwazukia wenye adili gizani;
Ana fadhili na huruma na haki.
5 # Lk 6:35 Heri atendaye fadhili na kukopesha;
Atengenezaye mambo yake kwa haki.
6Kwa maana hataondoshwa kamwe;
Mwenye haki atakumbukwa milele.
7Hataogopa habari mbaya;
Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.
8Moyo wake umethibitika hataogopa,
Hata awaone watesi wake wameshindwa.
9 # Lk 11:41; Rum 12:13; Mdo 4:35; 20:35; 2 Kor 8:9; 9:9; 1 Tim 6:18 Amekirimu, na kuwapa maskini,
Haki yake yakaa milele,
Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.
10 # Lk 13:28 Asiye haki ataona na kusikitika,
Atasaga meno yake na kuyeyuka,
Tamaa ya wasio haki itapotea.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 112: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha