Tumetenda dhambi sisi na wazee wetu; tumetenda maovu, tumefanya mabaya. Wazee wetu walipokuwa Misri, hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu; hawakukumbuka wingi wa fadhili zake, bali walimwasi kando ya bahari ya Shamu. Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi, ili aoneshe nguvu yake kuu. Aliikemea bahari ya Shamu ikakauka; akawapitisha humo kama katika nchi kavu. Aliwaokoa mikononi mwa waliowachukia; aliwaokoa kutoka kwa nguvu za maadui zao. Maji ya bahari yaliwafunika maadui zao; wala hakusalia hata mmoja wao. Hapo watu wake wakaamini maneno yake, wakamwimbia tenzi za sifa yake.
Share
Read Zaburi 106
Save verses, read offline, watch teaching clips, and more!
YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy
Home
Bible
Plans
Videos