Hasira ya Mwenyezi-Mungu ikawawakia watu wake, akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake. Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa, hao wenye kuwachukia wakawatawala. Maadui zao waliwakandamiza, wakawatumikisha kwa nguvu. Mara nyingi Mungu aliwaokoa watu wake, lakini wao wakachagua kumwasi, wakazidi kuzama katika uovu wao. Hata hivyo Mungu alizijali taabu zao, wakati aliposikia kilio chao; kwa ajili yao alilikumbuka agano lake, akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake. Aliwafanya waliowakandamiza wawaonee huruma. Utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa, tupate kulisifu jina lako takatifu, na kuona fahari juu ya sifa zako. Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele! Na watu wote waseme: “Amina!” Asifiwe Mwenyezi-Mungu!
Share
Read Zaburi 106
Save verses, read offline, watch teaching clips, and more!
YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy
Home
Bible
Plans
Videos