Kisha wakajiunga kumwabudu Baali kule Peori, wakala tambiko zilizotambikiwa mizimu. Waliichochea hasira ya Mwenyezi-Mungu kwa matendo yao, maradhi mabaya yakazuka kati yao. Lakini Finehasi akasimama kufanya malipizi, na yale maradhi yakakoma. Jambo hilo lakumbukwa kwa heshima yake, tangu wakati huo na nyakati zote. Walimkasirisha Mungu penye maji ya Meriba, Mose akapata taabu kwa ajili yao. Walimtia Mose uchungu rohoni, hata akasema maneno bila kufikiri. Hawakuwaua watu wa mataifa mengine kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru. Bali walijumuika na watu wa mataifa, wakajifunza kutenda mambo yao. Waliabudu sanamu za miungu yao, nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza. Waliwaua watoto wao wa kiume na wa kike, wakawatoa tambiko kwa pepo. Walimwaga damu ya wasio na hatia, damu ya watoto wao wa kiume na wa kike ambao waliwatoa tambiko kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikatiwa unajisi kwa mauaji hayo. Hivyo wakafanywa najisi kwa matendo yao, 2wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazinzi.
Share
Read Zaburi 106
Save verses, read offline, watch teaching clips, and more!
YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy
Home
Bible
Plans
Videos